Sakata la Dowans

Written By Admin on Thursday, September 29, 2011 | 2:16 PM

Tanzania: Sakata la Dowans

Watanzania wakabiliwa na mgao wa umeme
 
Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya kuridhia malipo ya fidia ya fedha kwa Kampuni ya ya Dowans ambayo ilisajili,tuzo yake iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC).
Kufuatia uamuzi huo  Shirika la umeme Tanzania Tanesco sasa linatakiwa liilipe Dowans kiasi cha Sh111 bilioni, badala ya Shilingi 94 bilioni za awali ikiwa ni pamoja na riba ya asilimia 7.5.

Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe, amesema hukumu hiyo ni matokeo ya wanasiasa  kutofuata ushauri wa kitaalam na kuweka mbele maslahi ya kisiasa.

0 comments:

Post a Comment