ALBUM YA IVETA

Written By Admin on Wednesday, August 18, 2010 | 6:26 PM

Album ya IVETA ya msanii SAJNA ina jumla ya nyimbo 10, ambayo ilianza kutengenezwa Mwezi January 2010 na kukamilika mwezi July 2010. Wasanii waliopata nafasi ya kushirikishwa katika album hii ni Belle 9, Linah wa THT, Josefly kutoka Musoma Mara pamoja na Pipi. Lengo la kutoshirikisha wasanii wengi sana ni kutaka kuonesha uwezo wake na kuthibitisha kwamba msanii mchanga si lazima atoke kwa kupitia mgongo wa wasanii wakubwa.

Studio na producers waliohusika kutengeneza nyimbo katika album hii ni pamoja na TETEMESHA RECORDZ chini ya KID BWOY, AB RECORDS chini ya AMBA, A2P chini ya SAM TIMBER, IMMORTAL MUSIC chini ya TRIS na M LAB chini ya DUKE.
Single ya pili kutoka bado haijaamuliwa ila ni kati ya SITAKI KUUMIZWA na MBALAMWEZI, moja kati ya hizo itakayopendekezwa na wadau wengi ndio itakayofuata baada ya IVETA.
NYIMBO ZILIZOPO KATIKA ALBUM
1. IVETA
2. Sitaki Kuumizwa ft. Linah
3. Binadamu
4. Mbalamwezi
5. Udehule
6. Mganga ft. Josefly
7. Nadhifa
8. Roho Mbaya ft. Belle 9 & Pipi
9. Subira
10.Ishara ya Msalaba

0 comments:

Post a Comment