TANZANIA yagoma Kutambua Waasi Libya

Written By Admin on Thursday, September 1, 2011 | 10:50 PM

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amesema Serikali ya Baba Riz haitakurupuka kuitambua serikali ya mpito ya  waasi wa Libya wakati bado vita inaendelea. 

 


Kwa mujibu wa Membe, nchi za Afrika ziizoitambua serikali ya waasi wa Libya ni pamoja na Kenya, Botswana, Ethiopia, Djibut, Rwanda na Tunisia.  Nyingine ni Senegal, Gabon, Gambia, Bokina Faso, Benin na Nigeria.  Alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi 41 za Afrika ambazo bado hazijaitambua serikali ya mpito ya waasi wa  Libya.

Membe alisema Serikali ya Baba Riz inajua kwamba hatima ya Kanali Muammar Gaddafi kuongoza Libya imekwishafikia, lakini haiwezi kuwatambua waasi wakati bado hawajaunda serikali.   “Serikali ni pamoja na kuwa na viongozi walioapishwa,  tutawatambua kama watakuwa na  mihimili mitatu ya serikali, bunge na mahakama,” alisema Membe.

0 comments:

Post a Comment